Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-, Kamanda wa Makao Makuu ya Kati ya Khatam al-Anbiya (s.a.w), Jenerali Ali Abdullahi, amezitaka nchi za eneo la Mashariki ya Kati kuwa makini na sera za ulinzi zinazowategemea mataifa ya kigeni, hususan Marekani.
Jenerali Abdullahi amesema kuwa nchi yoyote itakayomfanya Marekani kuwa ngao yake ya ulinzi inaweza kujikuta ikiingia katika madhara ya vita na migogoro.
Akizungumza kuhusu hali ya usalama katika eneo hilo, alieleza kuwa nchi za Kiislamu zinapaswa kufahamu kuwa Marekani, kwa kutumia rasilimali zao za kifedha, utajiri wao, miundombinu muhimu na uwezo wao wa kimkakati, hujenga mazingira ya kulinda maslahi yake ya kijeshi.
Aliongeza kuwa kwa mtazamo wake, baadhi ya mataifa makubwa hutumia uwezo na rasilimali za nchi za eneo hilo kuimarisha mipango yao ya kijeshi na kuunga mkono washirika wao wa kikanda.
Jenerali Abdullahi amesisitiza umuhimu wa nchi za eneo hilo kutegemea uwezo wao wenyewe, kudumisha umoja na kuzingatia usalama wa pamoja badala ya kutafuta ulinzi kupitia nguvu za nje.
Maoni yako